BONANZA LA MIAKA 15 YA UDOM SACCOS LTD


Jan. 8, 2026, 6:50 a.m.          Ericko Mwalongo



Katika kuadhimisha miaka 15 tangu kuanzishwa kwa chama cha ushirika wa akiba na mikopo chuo kikuu cha Dodoma (UDOM SACCOS LTD), uongozi umeandaa bonanza la michezo litakalohusisha wanachama, viongozi, watendaji, pamoja na wadau wote wa UDOM SACCOS LTD. Lengo likiwa ni kuonesha mshikamano, mchangamano na afya bora kupitia michezo, sambamba na kutoa burudani kwa jamii.

MICHEZO ITAKAYOSHINDANIWA NI: -

I. Mpira wa miguu

II. Netiboli

III. Kukimbia

IV. Kuvutana kwa Kamba

V. Mchezo wa bao la Kiswahili

VI. Kukimbia na Magunia

VII. Kufukuza Kuku

VIII. Mpira wa Wavu

IX. Rede

X. Kupanga Glass

XI. Drafti

XII. Kucheza karata

 

Bonanza hili litafanyika tarehe 10/1/2026 katika viwanja vya michezo CIVE – UDOM kuanzia saa 12:00 Asubuhi hadi saa 7:00 Mchana, pia kutakuwa na supu, nyamachoma na huduma nyingine. Ewe mwana michezo Wasiliana nasi kupitia nambari 0752085279 Wanachama na wadau wote mnakaribishwa sana kushiriki Bonanza hili “UDOM SACCOS LTD,

 

"Kwa Pamoja Tunatimiza Malengo Yako"

Habari na Matukio